Tuesday, November 27, 2012

KIFO CHA STEVEN KANUMBA, MARIAM KHAMIS, JOHN MAGANGA, MLOPELO NA SHARO MILLIONEA JE,TUNAJIFUNZA NINI?

Jumatatu ya tarehe 26 Novemba, 2012 majira ya saa tatu na robo hivi, nikiwa nyumbani kwangu naangalia runinga, nilipata taarifa kuwa msanii maarufu wa vichekesho na muziki Hussein Ramadhan almaarufu kama Sharo Millionea amefariki dunia kwa ajali ya gari. Kusema ukweli, sikuamini kabisa kile nilichokisikia. Kadri muda ulivyozidi kwenda, ndivyo ambavyo meseji zinazohusu kifo cha msanii huyu zilivyozidi kumiminika katika simu yangu. Nililazimika kuingia mtandaoni na kutafuta ukweli wa jambo hili ndipo nilikutana na taarifa za kuwa kweli msanii huyu amefariki katika mtandao mmoja wa kijamii. Moyo wangu uliruka, kichwa kikanivimba, nikahisi mwili wangu kuishiwa nguvu.
"Ni nini?". Ndilo swali ambalo nilijiuliza mwenyewe na nikashindwa kujipatia jibu. Kwa sekunde kadhaa, nikajikuta nakumbuka matukio ya vifo vya wasanii kadhaa ambavyo vilitokea nyuma ndani ya mwaka huu na tena vingine vikipishana kwa siku chache tu. Bila kutegemea, nilijikuta nikishikwa na kwikwi na machozi kunitiririka kama maji. Mbona ni vijana wadogo ambao kila mmoja alikua na ndoto za kufika mbali?. Lakini baada ya kulia mwenyewe kwa muda, nilikumbuka neno la "KILA NAFSI ITAONJA MAUTI".  Nilipokumbuka hilo, nilisema Amina kisha nikafuta machozi na kuanza kutafakari kwa kina juu ya vifo vya wasanii hawa, Kanumba, Mariam Khamis, Mlope, John Maganga na sasa Sharo Millionea. Neno kwanini?, kwanini? lilishika nafasi kichwani mwangu. Baadae nikajiulizia mwenyewe, au ni sauti ya Mungu? Ni Mungu anazungumza nasi kwa njia hii ili tukumbuke kuwa yupo?. Nilijitafakari mara mbilimbili kwa kujiuliza kuwa, hawa wenzetu wamekwenda na sisi tupo nyuma yao, je, Mwenyezi Mungu akiniita mimi Teddy leo hii, nitakwenda wapi?
Pengine niseme tu kwamba, vifo vya wapendwa wetu hawa, viwe funzo kwetu. Viwe funzo kwetu kwa maana kwamba, sisi kama binadamu tuishi tukijua kwamba, Mungu yupo na kifo hakichagui mtoto, kijana au mzee. Mungu akimpenda yeyote humchukua wakati wowote.
Ni vema sasa kila mmoja wetu atafakari mtindo wa maisha anaoishi. Tuishi maisha yanayompendeza Mungu kila mmoja kwa imani yake ili basi tutakapoitwa, tuwe tayari kwa maisha mapya tuliyoahidiwa.
Mwenyezi Mungu na azilaze roho za marehemu hawa wote mahali pema peponi, Aamina.
Sisi tuliwapenda lakini Mwenyezi Mungu amewapenda zaidi.
Ashleymama.com.

WMA- UYUMBU, THE PROUD OF URAMBO

 
 UYUMBU ni Jumuia ya Hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori ambayo ipo katika Kata ya Uyumbu, Tarafa ya Ussoke Wilayani Urambo.
Jumuia ina ukubwa wa eneo la km 838.7. Aidha, Jumuia hii, ina haki ya kutumia raslimali zilizomo ndani ya hifadhi hiyo ambazo ni  uwindishaji wa Kitalii, upigaji picha, uwindaji wa kienyeji, uvuvi na uvunaji wa asali na mbao.
Tarehe 19 Novemba, 2012 Waheshimiwa Madiwani Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mhe. Haruna Kasele, walifanya ziara ya kwenda kuitembelea Jumuia hii ili kujionea shuguli mbalimbali zinazoendeshwa katika eneo hilo. Ashleymama.com, ilipata bahati ya kuongozana na Waheshimiwa hao katika safari hiyo. Safari ilikua ndefu na ya kuchosha lakini baada ya kufika katika hifadhi hiyo, kamwe sikujuta kwa sababu ya mambo mazuri ya kufurahisha na kupendeza ambayo tuliyakuta kule. Kwakweli, sikuweza kuamini kama eneo lile lipo Urambo lakini ukweli bado unabaki palepale kwamba hifadhi hii ipo Urambo na Watalii kutoka nchi za nje hufika katika hifadhi hii kwa ajili ya kuangalia wanyama na kuwinda. Na pengine nikujuze kuwa, hata mfalme wa jumuia za kiarabu amewahi kufika katika hifadhi hii. It si so wonderful my dear.
Mi nisikumalizie uhondo, ngoja nikushushie picha moja baada ya nyingine ili ili uweze kuona jinsi tulivyokula bata wenzenu.
 
                                         
                                   Wajumbe wakisikiliza maelekezo kutoka kwa wenyeji wa hifadhi
 
                                    
 
                                                      Mandhari ya hifadhi ya WMA
 
 
                                                                           Mto Walla
 
                                         Waheshimiwa Madiwani wakiwa wametulia .
 
 
Waheshimiwa wakibadilishana mawazo 
 
 
                            Mkurugenzi wa ABUSAT Bw. Hilal Soud akitoa maelezo kwa Wajumbe
 
 
 
                 Kushoto ni Mkurugenzi wa Ashleymama.com Bi Teddy Chacha na Kaimu Afisa Elimu (S) Bi. Grace Monge
 
 
                                 
                                         
 
                            Mojawapo ya nyumba za kulala wageni wanaofika katika eneo hilo
 
            
                             Mhe. Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. H. Kasele akiwa amejiachia kwa raha zake kitandani
 
             
 
 Woouw!Nice room
 
              
 Chinekeee!Mtoto wa kikulya mie,  mate yananidondoka kwa uchu wa nyama yarabi
                
 
Tobaa mie yarabi, Daaah!
           
 
    Wajumbe wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa ABUSAT Bw. Hilal Soud 
 
Kwakweli, tuliinjoi sana. Hivyo Mtanzania mwenzangu, ukipata nafasi hebu fika mahali hapa ukajionee mwenyewe. Usisubiri kuhadithiwa.
Bahati mbaya ni kwamba, kwa muda tuliokua tumekwenda, ni muda ambao wanyama huwa wamejipumzisha hivyo hatukuona wanyama kivileeee. Ila tuliwaona ila Kamera ya ashleymama.com haikuweza kuwafikia. Walikua mbali halafu walikua wakiona gari wanakimbia. Waoga haoooo.
 
Asanteni na Karibu tena.
Ashleymama.com.